Karibu

Chama Cha Sarufi ya Kiswahili Tanzania kwa Sarufi. Uchambuzi. Semina. Mafunzo. Makala.

CHASAKITA ni chama kilichoanzishwa kwa lengo la kukuza, kulinda na kuendeleza Sarufi ya Kiswahili nchini Tanzania na nje ya nchi. Kuanzishwa kwake kulitokana na changamoto za Sarufi ya Kiswahili kuonekana kuwa ngumu kwa wanafunzi na walimu pamoja na kutokuwa na nafasi kubwa katika soko la ajira. Chama hiki kinalenga kusimamia maendeleo ya Sarufi ya Kiswahili katika sera, mitaala na ufundishaji ili kuimarisha matumizi na hadhi yake.

Makala yote
Slider Image

MAJUKUMU YA CHASAKITA

Kuikuza na kuieneza sarufi ya Kiswahili

Kwa kushiriki mihadhara semina na makongamano

Kuendesha shughuli za kitaaluma,

kijamii na kitamaduni kuhusu Sarufi na Isimu ya Kiswahili.

Kujenga uhusiano na kushirikiano

Hasa na asasi nyingine za kitaifa, kikanda na kimataifa zinazounga mkono uendelezaji wa Kiswahili.

Kuhimiza ufundishaji na usomaji wa taaluma mbalimbali,

Kama tafsiri na ukalimani, pamoja na kuimarisha shughuli hizo

Kutoa mafunzo ya muda mfupi

Ili kuongeza uchechemuzi wa kisarufi kwa watumiaji wa lugha ya Kiswahili.

Kutoa mafunzo ya kufundisha Kiswahili kwa wageni.

Mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi

Ujumbe wa Mwenyekiti

Mahenda Kulwa Jagadi -Mwenyekiti na Muasisi -CHASAKITA

Mahenda Kulwa Jagadi -Mwenyekiti na Muasisi -CHASAKITA

Ndugu wanachama, wadau wa lugha ya Kiswahili, walimu, wanafunzi na jamii kwa ujumla, Napenda kukukaribisheni katika Chama cha Sarufi ya Kiswahili Tanzania (CHASAKITA), taasisi iliyoanzishwa kwa dhamira ya kuenzi, kulinda na kuendeleza Sarufi ya lugha ya Kiswahili sanifu nchini Tanzania na nje ya mipaka yake. CHASAKITA imeanzishwa kutokana uhitaji mkubwa wa kuwa na chombo maalumu kitakachofuatilia kwa karibu maendeleo ya Sarufi ya Kiswahili kuanzia ngazi ya elimu ya msingi hadi elimu ya juu, pamoja na matumizi yake katika jamii na taasisi mbalimbali. Kwa muda mrefu, Sarufi ya Kiswahili imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo kuonekana kuwa ni ngumu kwa wanafunzi na baadhi ya walimu, kudunishwa hadhi yake, pamoja na .... ...

Chama Cha Sarufi ya Kiswahili Tanzania-CHASAKITA

Matarajio makuu ya CHASAKITA ni kuhakikisha kuwa walimu wa sarufi ya Kiswahili na jamii wanapata elimu ya kutosha kuhusiana na mambo muhimu katika kuenzi, kutunza na kuendeleza sarufi ya lugha ya Kiswahili ili kusaidia uwepo wa jamii ambayo itakuwa na mabadiliko na mitazamo mipya na hatimaye kutokuwa na jamii iliyo na mitazamo hasi juu ya sarufi ya lugha na kufanikisha uwepo wa jamii itakayoenzi, kutunza na kuendeleza sarufi ya lugha ya Kiswahili na tunatarajia kuwa, jamii itaweza kujivunia sarufi ya lugha ya Kiswahili ndani na nje ya Tanzania..

Ungana nasi

Matarajio

kuhakikisha kuwa walimu wa sarufi ya Kiswahili na jamii wanapata elimu ya kutosha kuhusiana na mambo muhimu katika kuenzi, kutunza na kuendeleza sarufi ya lugha ya Kiswahili

Malengo

Kuimarisha misingi ya sarufi ya Kiswahili kwa walimu wa Kiswahili nchini ili kuongeza uelewa na ari ya kutaka kuienzi, kuitunza na kuieneza sarufi ya Kiswahili

Msingi

kukuza na kuendeleza sarufi ya Kiswahili sanifu kitaifa na kimataifa kupitia mafunzo ya kitaaluma, warsha, uandishi na uchapishaji.

Taarifa Mpya

No results found...

Shughuli za mawanda

678

Semina

422

Warsha

1621

Wanachama

865

Wanachama wapya

Viongozi Waandamizi

Maendeleo ya CHASAKITA yanachagizwa na wanachama pamoja na viongozi mahiri.

Mwenyekiti

Profile Image
Mahenda K.Jagadi
Mwenyekiti

M/kiti-Kamati tendaji

Profile Image
Tumaini M. Nginila
Makamu M/Kiti

Katibu

Profile Image
Bimkubwa Swalehe
Katibu

Mhazini

Profile Image
Tuladega Tweve
Mhazini

Kwa ushauri na maoni wasiliana nasi kwa kubonyeza kitufe hapo

..